Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) linaungana na dunia nzima kuenzi kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Malkia Elizabeth II, aliyezaliwa Aprili 21, 1926.
Hayati Malkia Elizabeth II alihudumu kama kiongozi wa kifalme wa Uingereza na Mkuu wa Nchi katika mataifa kadhaa ya Jumuiya ya Madola kwa zaidi ya miongo saba, akionesha uongozi uliotukuka uliojengwa juu ya uadilifu, uwajibikaji na kujitolea kwa wananchi wake na dunia kwa ujumla.
Kwa sasa, nafasi hiyo inaendelea kushikiliwa na Mfalme Charles III, ambaye anaendeleza urithi wa uongozi wa kifalme kwa kuhimiza mshikamano wa kimataifa na maendeleo endelevu.
Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) Boniventura Mwalongo ambapo amesema katika kuenzi tarehe hiyo muhimu ya 21 Aprili, dunia pia shirika hilo inawakumbuka watu wengine mashuhuri waliozaliwa siku hii, wakiwem


0 Comments