About Me

header ads

TMDA YAPONGEZWA KWA KUDHIBITI DAWA,KUJENGA MAKAO MAKUU YA KANDA TABORA

 

Na Emmanuel Massaka,Tabora

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA) imepongezwa kwa kazi kubwa ya udhibiti wa dawa nchini sambamba na ujenzi wa makao makuu ya kanda ya TMDA katika Mkoa wa Tabora ambayo ni heshima kubwa ya Mkoa huo.

Pongezi hizo zimetolewa leo Julai 16,2025 na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paulo Chacha alipokuwa akifungua kikao kazi cha wahariri kilichofanyika mjini Tabora ambapo pia ameeleza wamejipanga kuhakikisha hati miliki ya kiwanja inatolewa haraka ili kuruhusu ujenzi wa jengo hilo uanze.

Chacha amesema kwamba Tabora ina umuhimu wa kimkakati kutokana na kupitiwa na reli ya kisasa (SGR) huku akifafanua kuwa maboresho makubwa katika sekta ya afya yamefanyika chini ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan .


Ametaja maboresho hayo ni yamehusisha kuimarisha taasisi kama TMDA na hiyo ni hatua muhimu kwa ustawi wa afya ya jamii ya Watanzania.

Mkuu wa Mkoa huo ametumia nafasi hiyo kuelezea  wasiwasi wake kuhusu ongezeko la matangazo holela ya dawa za binadamu, hivyo ametoa mwito kwa TMDA kushirikiana na vyombo husika kudhibiti hali hiyo. 

“Pia ni vema wafanyabiashara wakaelemishwa kuhusu madhara ya dawa na vifaa tiba bandia na duni ambavyo si salama kwa matumizi ya binadamu.”
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt Adam Fimbo, ametangaza kwamba  TMDA kwa kushirikiana na taasisi nyingine inaendesha utafiti maalumu kubaini kiwango cha matumizi ya dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI (ARVs) katika utambuzi wa mifugo, jambo linaloibua hofu ya usalama wa afya kwa walaji.

Ameongeza baada ya utafiti huo  kukamilika, watakuwa katika nafasi nzuri ya kuchukua hatua stahiki kudhibiti tatizo hilo.

Kuhusu kikao cha wahariri amesema lengo la kikao hicho ni kuongeza uelewa wa wahariri kuhusu majukumu ya TMDA na kuonyesha mafanikio ya taasisi hiyo katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita.Ametaja baadhi ya  mafanikio hayo ni pamoja na usajili wa jumla ya dawa 8,332 katika kipindi hicho, hatua iliyosaidia kupanua upatikanaji wa dawa muhimu kwa wananchi.

Wakati huo huo Joyce Shebe aliyekuwa Mwenyekiti wa kikao hicho cha wahariri na TMDA amesema uamuzi wa mamlaka hiyo kuwaalika kwenye kikao hicho ni hatua muhimu inayowapatia maarifa yatakayotuwezesha kuandika kwa ufanisi zaidi kuhusu masuala ya afya












 

Post a Comment

0 Comments