
Mkuu wa Wilaya Rombo, Raymond Mwangwala (watatu kulia) akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 10 kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru (wapili kushoto) kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa uzio wa Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Sambambama na hilo, pia Benki ya CRDB imekabidhi madawati 111 yenye thamani ya shilingi milioni 10, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuchangia maendeleo ya jamii kupitia uwekezaji unaolenga sekta muhimu za afya, elimu na mazingira ambayo asilimia 1 ya faida baada ya kodi hutengwa kila mwaka kwa ajili ya kusaidia miradi ya kijamii yenye tija. Mchango huu unalenga kuhakikisha ushiriki wa Benki ya CRDB katika kukuza elimu na kuboresha mazingira ya kusomea yaliyo salama. Wengine pichani ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat (kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rombo, Emmanuel Sindiyo (kulia) pamoja na Afisa Tawala wa Rombo, Isack Martin.

Mkuu wa Wilaya Rombo, Raymond Mwangwala (kulia) akipokea moja ya madawati kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru kwa ajili ya Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro. Kushoto ni Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat.


Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya CRDB Bank Foundation, Coletha Ndunguru akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Kaskazini, Cosmas Sadat akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika hafla hiyo, iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Prof. Adolf Mkenda iliyopo wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.

Burudani pamoja na wanafunzi



0 Comments