About Me

header ads

ANAYEFANYA KAZI BILA 'PRESS CARD' ANAVUNJA SHERIA- Prof. KABUDI

 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari. 

Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika leo tarehe 14 Julai, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Phillip Mpango jijini Arusha.

Amesema Press Card aliyopewa siyo kwa hisani bali ni kutokana na kukidhi vigezo, akiwa amewasilisha vyeti vya taaluma ya Uandishi wa Habari kwenye mfumo wa Bodi, huku akiwasisitiza Waandishi wengine kujisajili katika mfumo wa TAI-HABARI.

Waziri Kabudi amemuhoji Katibu Mtendaji Mstaafu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) ambao ni wenyeji wa Mkutano huo, Bw. Kajubi Mukajanga kama ameshajisajili na kupata Press Card, ambapo amekiri kuwa bado lakini atafanya hivyo siku chache zijazo nyaraka zake zikikamilika.

Mkutano wa Mabaraza la Habari Afrika unafanyika kwa mwaka wa pili nchini Tanzania ukitanguliwa na Mkutano wa kwanza uliofanyika Mwaka jana nchini Afrika Kusini.

Post a Comment

0 Comments