About Me

header ads

RAIS MWINYI:ZANZIBAR INA SERA BORA KWA UWEKEZAJI

 


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa ya maendeleo kipindi cha miaka 4 kwa mageuzi katika sekta mbalimbali na kuimarika kwa mifumo  pamoja na kuanzisha sera bora kwa uwekezaji zinazolenga kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na kimataifa. 

Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo katika Jukwaa la uwekezaji katika uchumi wa buluu lililofanyika katika Makao makuu ya Ofisi za Citibank, London tarehe 8 Aprili 2025 na kuhudhuriwa na Kampuni mbalimbali za uwekezaji za  Uingereza zenye nia ya kuchangamkia fursa za uwekezaji Zanzibar.

Aidha,  Rais Dkt.Mwinyi amefahamisha  kuwepo kwa  Citibank kuwa mshirika mkuu wa maendeleo Zanzibar kutachochea zaidi uwekezaji katika sekta za  uchumi wa buluu, nishati , pamoja na nyumba na makaazi.

 Halikadhalika,  Rais Dkt.Mwinyi amesema  ushirikiano kati ya sekta binafsi na umma unalenga kuzifanya bandari  kuwa za kisasa, uanzishwaji wa viwanda vya usindikaji  wa mazao ya baharini.

Vilevile Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa upatikanaji wa fedha utaisaidia Serikali kuendelea kuwawezesha Wanawake wakulima wa Mwani, wavuvi  na vijana  katika mafunzo  ya ujuzi mbalimbali.

Kwa upande mwingine,  Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito katika jukwaa hilo  kuwekeza katika sekta ya uvuvi na ufugaji wa samaki, utalii wa mazingira, na uhifadhi wa baharini.

Post a Comment

0 Comments